KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, March 6, 2010

Utaratibu kurudiana Ligi Kuu wapingwa




Bodi ya Ligi Kuu ya England imesema haiafiki utaratibu unaopendekezwa wa mechi za marudiano kwa ajili ya kufuzu kwa mshindi wa nne na timu itakayopata nafasi pia ya kucheza Ligi ya Mabingwa wa Ulaya.
Katika mkutano wa bodi hiyo uliofanyika siku ya Alhamisi, mwenyekiti wake aliamua kupinga pendekezo hilo kwa wakati wowote ule siku za baadae.

Manchester United, Chelsea, Liverpool na Arsenal imearifiwa nao haraka wamepinga wazo hilo.

Hata hivyo vilabu vingine kimsingi vinaelekea kuafiki wazo hilo

No comments:

Post a Comment