KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, February 20, 2010

Yar'Adua kusalia kuwa rais wa Nigeria




Baraza la mawaziri nchini Nigeria limepinga mswaada uliolenga kumondolea mamlaka rais Umaru Yar'Adua kwa msingi kuwa anaugua kiasi cha kutoweza kuongoza nchi tena.
Waziri wa habari Dora Akunyili amesema baraza limeamua badala yake, kutuma tena ujumbe mwingine nchini Saudi Arabia kumjulia hali rais Yar'Adua ingawa hakusema ni lini ujumbe huo utaondoka.

Rais Yar'Adua anaendelea kupokea matibabu nchini Saudi Arabia kwa zaidi ya miezi mitatu sasa.

Thuluthi mbili ya wabunge wa Nigeria ndio wanaweza kupitisha mswaada kama huo . Wiki iliopita makamu wa rais Goodluck Jonathan, alichukua wadhifa wa kaimu rais kufuatia agizo la bunge.

No comments:

Post a Comment