KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, February 20, 2010

ARV'S zazuia maambukizi ya HIV


Utafiti mpya umeonyesha kuwa dawa zinazotumika kutibu maradhii tegemezi kwa wagonjwa wa ukimwi (ARVS) zinaweza kuzuia maambukizi ya virusi vya HIV.
Utafiti uliofanywa miongoni mwa wanandoa elfu tatu mia tano wanaogua virusi hivyo barani afrika , ulionyesha kuwa uwezekano wa wagonjwa waliotumia sana dawa za ARV,'s kuwaambukiza wenzao, ni wa chini mno.

Kwa kipindi cha miaka mitatu, zaidi ya visa mia moja vya maambukizi mapya ya HIV viliripotiwa miongozi mwa waliokuwa wanafanyiwa utafiti huo. Lakini ni mtu mmoja tu aliyekuwa anatumia dawa hizo ndiye alieambukizwa.

Waliofanya utafiti huo, wanasema huenda mtu huyo aliambukizwa kutokana mabadiliko mwilini mwake yaliosababishwa na dawa hizo.

No comments:

Post a Comment