KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, February 20, 2010

UN yaikosoa Marekani kuhusu Somalia




Umoja wa mataifa unasema masharti yaliyowekwa na Marekani ya kutoa msaada kwa Somalia yanasababishia raia mateso makubwa.
Mratibu wa misaada ya kibinadamu nchini Somalia Mark Bowden ameilaumu Marekani kwa kuligeuza swala la msaada kuwa la kisiasa katika juhudi zake za kuhakikisha misaada haiwafikii wanamgambo wa Kiislamu wanaodhibiti eneo kubwa la nchi.

Umoja wa mataifa unakadiria kwamba katika eneo moja la Somalia , asilimia 70 ya watu wanahitaji msaada wa chakula ili kuendelea kuishi.

Lakini Bw Bowden amesema mashirika ya kimisaada hayawezi kutimiza masharti yaliyotolewa na Marekani ambayo ndio mfadhili mkuu wa misaada nchini Somalia.

No comments:

Post a Comment