KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, February 9, 2010

Wanajeshi 15 wa India wameuwawa mapema jana Jumatatu


Maporomoko ya barafu yaua 15 Kashmir

Kashmir.

Wanajeshi 15 wa India wameuwawa mapema jana Jumatatu wakati maporomoko makubwa ya barafu yalipofunika kituo cha mafunzo ya jeshi katika mji wa kitalii katika eneo linalodhibitiwa na India la Kashmir. Msemaji wa jeshi amesema kuwa maporomoko hayo yalikifunika kituo hicho cha jeshi kilichoko milimani kiasi saa tano asubuhi na kuporomoka na wanajeshi hao wakati wakiwa katika mafunzo. Watu 17 pia wamejeruhiwa katika maporomoko hayo ya barafu. Eneo hilo , liko katika urefu wa mita 2,730, ambapo ni katika mpaka unaogawanya Kashmir , kati ya India na Pakistan. Waokoaji bado wanawatafuta wanajeshi wawili zaidi ambao hawajulikani waliko na wanahofiwa wamezikwa chini ya barafu.

No comments:

Post a Comment