KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, February 9, 2010

Muasi wa Darfur hatoshtakiwa ICC




Majaji katika mahakama ya kimataifa ya kivita ya ICC wamefuta mashtaka dhidi ya kiongozi wa waasi katika jimbo la Darfur.
Bahr Idriss Abu Garda alishutumiwa kwa mauaji ya wanajeshi 12 wa kutafuta amani mwaka 2007. Alijisalimisha mwenyewe mwaka uliopita.

Lakini majaji walitoa uamuzi kuwa hakuna ushahidi wa kutosha kwa kesi dhidi yake.

Wiki iliopita,mahakama ya ICC ilisema mashtaka ya mauaji ya kimbari dhidi ya rais wa Sudan Omar al-Bashir yanaweza kuwasilishwa tena.Al-Bashir anatakiwa na mahakama hiyo kwa makosa ya kivita.

No comments:

Post a Comment