KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, February 9, 2010

al-Shihri wa al-Qaeda alzishutumu Misr na Saudia.


al-Shihri wa al-Qaeda alzishutumu Misr na Saudia.

Sana'a.

Tawi la al-Qaeda nchini Yemen , kundi ambalo linadai kuhusika na jaribio lililoshindwa la kuilipua ndege ya shirika la ndege la Marekani siku ya Chrismass, limetoa wito wa mashambulio zaidi dhidi ya maslahi ya Marekani kila mahali. Katika ujumbe wa dakika 12 wa video uliotolewa katika mtandao wa internet, kiongozi wa pili wa al-Qaeda katika rasi ya Uarabuni, Said al-Shihri, pia ameishutumu Misr na Saudi Arabia kwa kusaidia kile alichosema kuwa ni Wakristo kupambana dhidi ya Uislamu katika rasi ya Uarabuni. Ameishutumu Saudi Arabia na Misr kwa kuhifadhi kile alichosema kuwa ni maslahi ya Wayahudi na Wakristo katika eneo hilo la rasi. Shihri, ambaye ni raia wa Saudi Arabia , alishikiliwa katika jela ya kijeshi la Marekani ya Guantanamo Bay, nchini Cuba, kwa muda wa karibu miaka sita.

No comments:

Post a Comment