KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, February 6, 2010

Wamishonari mahakamani Haiti




Wamishonari kumi raia wa marekani wamefikishwa mahakamani kwa madai ya kuwateka nyara watato nchini Haiti.
Raia hao walishtakiwa kwa kujaribu kuwasafirisha watoto nje ya nchi hiyo baada ya tetemeko kubwa la ardhi katika mji mkuu wa Port-Au_Prince.

Wengi wao walifunika nyuso zao na kuimba nyimbo za kidini wakati walipokuwa wakiondolewa mahakamani.

Washukiwa hao wanadai kuwa walikuwa wakiwapeleka watoto hao katika makao moja ya watoto ilioko nchi jirani ya Jamhuri ya Dominican.

No comments:

Post a Comment