KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, February 6, 2010

Uchaguzi wa Gavana kufanyika Anambra, Nigeria




Hali ya Ulinzi imeimarishwa katika jimbo la kusini mashariki la Anambra nchini Nigeria, siku moja kabla ya kufanyika uchaguzi wa gavana wa eneo hilo.
Waandishi wa Habari wanasema kuna hali ya wasi wasi kuhusu unachaguzi huo, unaoendeshwa na tume ya uchaguzi iliyosimamia uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2007, ambao ulighubikwa na wizi wa kura na udanganyifu.

Miongoni mwa masuala yanayozua utata ni pamoja na usajili wa wapiga. Wachunguzi wanasema matokeo ya uchaguzi huo wa Anambra, huenda utakatoa mwelekeo kuhusu shughuli za uchaguzi nchini humo miaka ijayo.

No comments:

Post a Comment