KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, February 12, 2010

Viongozi wa Rwanda watishia wakosoaji




Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema, serikali ya Rwanda inawashambulia na kuwatishia wakosoaji wa uongozi wa nchi hiyo inayoelekea kwenye uchaguzi wa Rais mwezi Agosti.
Shirika hilo limesema viongozi wanawalenga upinzani kwa madai kuwa walishiriki katika mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.

Msaidizi wa kiongozi wa upinzani amefungwa kwa uhalifu wa mauaji hayo, lakini amedai kuwepo nje ya nchi wakati huo.

Rais Paul Kagame amesema anaheshimu haki za watu lakini hatomvumilia yeyote anayevuruga amani na utulivu.

Hata hivyo, Human Rights Watch limesema vitisho kwa upinzani inavuruga demokrasia.

No comments:

Post a Comment