KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, February 12, 2010

Goodluck atikisa baraza la mawaziri Nigeria




Katika siku yake ya kwanza kama kaimu wa rais, Goodluck Jonathan ameongoza kikao cha baraza la mawaziri na kufanya mabadiliko katika baraza hilo.
Bwana Jonathan amemuondoa mamlakani mkuu wa sheria Michael Aondoakaa, na kumpa wadhifa wa mwingine serikalini.

Bwana Aondoakaa amekuwa akilaumiwa kwa kuzuia uchunguzi dhidi ya wanasiasa wanaokabiliwa na shutuma za ufisadi.

Bunge la Nigeria lilimkabidhi mamlaka mapema wiki hii. Amechukua nafasi ya Rais Umaru Yar'Adua, ambaye anaugua. Baraza la mawaziri limeridhia hatua hiyo, licha ya wasiwasi wa hapo awali kuhusu uhalali wake.

No comments:

Post a Comment