KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, February 12, 2010

Blatter atetea waandalizi wa kombe la dunia




Rais wa shirikisho la soka ulimwenguni, FIFA, Sepp Blatter, amewashutumu wanaokosoa kuandaliwa kwa kombe la dunia mwaka huu Afrika Kusini.
Rais wa klabu ya Bayern Munich ya Ujerumani, Uli Hoeness, amenukuliwa akisema FIFA, ilifanya kosa kubwa kuipa Afrika Kusini nafasi ya kuandaa mashindano hayo. Lakini Blatter amesema matamshi hayo ni ya kudunisha bara la Afrika na hayana msingi wowote.

Kocha wa klabu ya Hull City, Phil Brown amesema kushambuliwa kwa timu ya Taifa ya Togo, wakati wa mashindano ya kombe la mataifa bingwa barani Afrika, nchini Angola, kunazua hali ya wasi wasi kwa timu zitakazoshiriki katika fainali ya kombe la dunia nchini Afrika Kusini.

Watu wawili waliuwawa, waasi waliposhambulia basi la timu hiyo katika eneo la Cabinda. Lakini Blatter amesema tukio hilo lililotokea nchini Angola halina uhusiano wowote na maandalizi ya kombe la dunia.

No comments:

Post a Comment