KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, February 6, 2010

Shangaziye Obama ajitetea mahakamani


Shangaziye Rais Barrack Obama, Zeituni Onyango amefika mbele ya mahakama moja mjini Massachussets, katika jaribio lake la pili, la kutafuta hifadhi ya kisiasa nchini Marekani.

Wakili wake amesema kesi ya Bi Onyango inazingatia misingi ya afya yake na hofu ya mapigano ya kikabila nchini Kenya. Bi Zietuni Onyango alijitetea faraghani.

Madaktari wawili pia walitoa ushahidi kwa niaba yake. Afisa wa idara ya habari katika Ikulu ya White House amesema Rais Obama, hajazungumza na shangaziye, tangu hatma yake ilipojulikana kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa urais.

No comments:

Post a Comment