KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, February 9, 2010

Uchaguzi ulikuwa wa haki; Wachunguzi




Kiev.

Nchini Ukraine, kiongozi wa upinzani Viktor Yanukovych ameibuka kuwa mshindi katika uchaguzi wa rais, akiendelea kuongoza kwa kiasi cha asilimia 3 wakati kiasi cha kura asilimia 99 zimekwisha hesabiwa. Wachunguzi wa kimataifa wameusifu uchaguzi huo kuwa ni huru na wa uaminifu, na kuimarisha madai ya ushindi ya Yanukovych na kumuacha waziri mkuu Yulia Tymoshenko akiwa amefungika kimkakati. Hata hivyo , waziri mkuu Tymoshenko bado anaendelea kuwa na wingi katika bunge la Ukraine, hali ambayo inaonekana kuendeleza mzozo katika utawala wa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment