KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, February 9, 2010

Serikali ya mamlaka ya Palestina imetangaza kuwa inatarajia kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa


Ramallah.

Serikali ya mamlaka ya Palestina imetangaza kuwa inatarajia kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa katika ukingo wa magharibi na ukanda wa Gaza Julai 17. Chama cha Hamas kimejibu haraka kwa madai kuwa mamlaka ya Palestina haina haki ya kuitisha uchaguzi. Uchaguzi wa mwisho uliofanyika 2006 ulikipatia chama hicho chenye nadharia za kidini cha Hamas ushindi katika miji mingi mikubwa katika maeneo yote kabla ya kuchukua udhibiti kwa nguvu katika ukanda wa Gaza 2007.

Uchaguzi wa serikali za mitaa Palestinian Julai.

Rais wa Palestina Mahmoud Abbas , alipanga uchaguzi ufanyike mwezi uliopita kwa mujibu wa katiba, lakini baadaye alitangaza kuuahirisha hadi Juni mwaka huu. Chama cha Hamas katika ukanda wa Gaza kimesema kuwa hakutakuwa na uchaguzi kabla ya chama cha rais Mahmoud Abbas cha Fatah kufikia makubaliano ya maridhiano na chama hicho.

No comments:

Post a Comment