KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, February 9, 2010

Mkuu wa zamani wa jeshi Sri Lankan akamatwa.


Mkuu wa zamani wa jeshi Sri Lankan akamatwa.

Colombo.

Mkuu wa zamani wa jeshi la Sri Lanka amekamatwa kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kosa la kijeshi kwa mujibu wa msemaji wa jeshi hilo. Jenerali Sarath Fonseka aliongoza awamu ya mwisho ya operesheni ambayo ilisababisha kushindwa kwa uasi wa kundi la Tamil Tigers mwaka jana kabla ya kuingia katika kinyang'anyiro cha uchaguzi wa urais akishindana na rais Mahinda Rajapaksa mwezi uliopita. Tangu kuchaguliwa tena kwa Rajapaksa majeshi ya usalama yamekuwa yakiwakamata wafuasi wa Fonseka. Jenerali huyo wa zamani mwenye nyota nne amepinga matokeo ya uchaguzi wa rais akisema kuwa anania ya kupinga matokeo hayo katika mahakama kuu.

No comments:

Post a Comment