KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, February 9, 2010

Benki ya Liechtenstein kuwalipa wakwepaji kodi hasara.


Benki ya Liechtenstein kuwalipa wakwepaji kodi hasara.

Vaduz, Leichtenstein.

Benki tanzu ya zamani ya benki ya LGT nchini Leichtenstein imeamuriwa kumlipa mkwepaji kodi wa Ujerumani euro milioni 7.3 katika hasara aliyopata . Mahakama nchini Leichtenstein imetoa hukumu kuwa benki hiyo ilichelewa kutoa taarifa kwa mteja wake kuwa data za mteja huyo zimeibiwa. Mdai amesema kuwa iwapo angearifiwa mapema, angeweza kuepuka faini ya euro milioni 7.3 inayotozwa kwa mkwepaji kodi. Mwajiriwa wa zamani wa benki aliiba na kuuza CD ambayo ina data za wateja kwa shirika la ujasusi la Ujerumani kwa kiasi cha euro milioni 4.5. Mmoja kati ya wakwepaji hao katika CD hiyo alikuwa mwenyekiti mtendaji wa huduma za posta nchini Ujerumani Klaus Zumwinkel.

No comments:

Post a Comment