KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, February 4, 2010

Misri wapanda chati

Mabingwa wa soka barani Afrika, Misri wamepanda ngazi katika orodha ya kumi bora ya shirikisho la kandanda la mataifa FIFA.
Kutokana na orodha iliyotolewa leo, Misri ndio timu inayoongoza kutoka Afrika ikishikilia nafasi ya 10.

Hii ndio nafasi ya juu kabisa kushikiliwa na timu ya Afrika tangu mwaka 1994 ambapo Nigeria ilishikilia nafasi ya tano.

Nigeria pia imepanda na inashiklia nafasi ya 15 duniani na ndio ya pili katika timu bora za Afrika.

No comments:

Post a Comment