KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, February 12, 2010

Afrika kusini yamuenzi Mandela


Raia wa Afrika Kusini leo wanaadhimisha miaka ishirini tangu alipoachiliwa huru Mzee Nelson Mandela.
Sherehe kubwa zitafanyika mjini Cape Town ambapo mke wa zamani wa Mandela, Winnie ataongoza maandamano hadi katika gereza ambalo alitumikia kifungo chake cha mwisho.

Mzee Mandela mwenye umri wa miaka 91 anatarajiwa kuonekana hadharani baada ya muda mrefu wakati atakapohudhuduria kwenye sherehe hizo ambapo Rais Jacob Zuma atahutubia taifa leo jioni.


Alitumikia kifungo kwa miaka 27 na baada ya kuachiliwa aliongoza mazungumzo yaliyosababisha kufanyika uchaguzi wa kwanza wa demokrasia. Katika uchaguzi huo Mzee Mandela alichaguliwa kuwa rais wa Kwanza mweusi nchini Afrika kusini mwaka wa 1994.

No comments:

Post a Comment