KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, February 20, 2010

China yaghadhabishwa na Marekani




Serikali ya china imeelezea kughadhabishwa na mkutano uliofanyika kati ya kiongozi wa kidini wa Tibet Dalai Lama na rais Barack Obama.
Saa chache tu baada ya mkutano huo, china, ambayo imekuwa ikisanifu mienendo ya kiongozi huyo wa kidini, ilisema kuwa mkutano huo ulikiuka sheria za kimataifa na sera za kigeni za marekani.

Imesema pia kuwa Marekani lazima ikome kuwaunga mkono maadui wake.

Baada ya mkutano huo msemaji wa Rais Obama ameelezea kuwa Obama alipongeza juhudi za Dalai Lama za kupinga mapinduzi kwa kutumia nguvu na badala yake kuegemea mashauriano na china.

No comments:

Post a Comment