KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, February 20, 2010

AU, ECOWAS zapinga mapinduzi Niger




Muungano wa kiuchumi wa nchi za Afrika magharibi ECOWAS umetuma ujumbe kwenda Niamey, mji mkuu wa Niger, kuelezea pingamizi za muungano huo kuhusu mapinduzi ya kijeshi yaliyomwondoa madarakani Rais Mamadou Tandja.
Msemaji wa ECOWAS amesema muungano huo unazingatia sera za kutokubali madaraka katika nchi yoyote kutwaliwa pasipo kufuata katiba ya nchi.

Umoja wa Afrika, AU, pia kupitia mwenyekiti wa tume ya AU Jean Ping umelaani mapinduzi hayo ya Niger.

Viongozi wa kijeshi walioipindua serikali ya Bw Tandja wameahidi kuigeuza nchi hiyo kuwa mfano bora wa nchi inayozingatia demokrasia na utawala bora.

Afisa mmoja wa ngazi za juu Kanali Salou Djibo ametangazwa kuwa kiongozi wa serikali ya kijeshi.

No comments:

Post a Comment