KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, February 20, 2010

Wamisri wakatazwa kumpokea ElBaradei


Vikosi vya kiusalama nchini Misri vimewazuia wafuasi wa upinzani kukusanyika katika uwanja wa ndege kumkaribisha aliyekuwa mkuu wa shirika la kimataifa la nguvu za Atomiki Mohammed ElBaradei, ambaye anakusudia kugombea Urais.
Wanaharakati wa upinzani wamekuwa wakitoa wito ElBaradei apewe makaribisho yanayostahiki shujaa, lakini mikutano ya hadhara sio halali nchini Misri na inaweza kuvunjwa na Polisi.

Bw ElBaradei alijenga sifa kubwa kimataifa alipokuwa mkuu wa shirika la IAEA , na alishinda tuzo ya Nobel mwaka 2005.

Anaonekana mwenye uwezo mkubwa wa kutoa upinzani kwa Rais Hosni Mubarak kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka ujao.

No comments:

Post a Comment