KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, January 18, 2010

Vita mjini Kabul, Taliban washambulia




Mapigano yamezuka katika mji mkuu wa Afghanistan kabul kati ya wapiganaji wa Taleban na wanajeshi wa nchi hiyo.
Mapigano hayo yametokea katika sehemu muhimu mjini humo iliyo na kasri la rais, jengo la benki kuu na wizara ya haki.

Mwandishi wa BBC mjini Kabul amesema kuwa amesikia milipuko na milio ya risasi karibu na majengo ya serikali.


Barabara zote kuu pamoja na mahoteli na majengo ya umma kufungwa katika eneo hilo. Kundi la waasi la Taliban limedai kuhusika na shambulio hilo.

No comments:

Post a Comment