KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, December 8, 2009

Maandamano Sudan kupinga Serikali




Waandamanaji nchini Sudan wameteketeza afisi za chama cha rais Omar Al Bashir zilizoko mji wa kusini kulalamikia kukamatwa kwa viongozi watatu wa chama cha SPLM.
Hakuna taarifa kuhusu waathirika katika majengo ya chama cha National Congress mjini Wau. Baadaye polisi waliwaachia huru wanasiasa hao.

Chama cha SPLM kilijiunga na serikali mwaka wa 2005 na kumaliza vita kati ya eneo la Kusini na Kaskazini.

Hata hivyo taharuki kati ya SPLM na washirika wao serikalini kutoka chama cha NCP imeendelea huku uchaguzi mkuu ukikaribia hapo mwakani.

Huu ndio uchaguzi mkuu wa kwanza kwa miaka 24 ambapo raia watamchagua rais, wabunge na wakuu wa mabaraza.

No comments:

Post a Comment