KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, November 27, 2009

Uchaguzi Namibia mashakani


Kampeni za uchaguzi nchini Namibia zimekumbwa na mizozo ya kisheria kabla ya kura za hapo kesho ijumaa.
Chama cha National Society for Human Rights kimewasilisha kesi kortini baada ya tume ya uchaguzi kuondoa hadhi yake ya msimamizi kwa madai kuwa na upendeleo.

Wakati huo huo chama kilichojitenga kutoka chama kikuu cha Swapo kimeiambia BBC kuwa kiongozi wake anadaiwa dollar za Marekani milioni kumi na tatu kwa kudai kuwa uchaguzi uliopita ulikuwa na dosari.



Mgombea wa chama cha Swapo akiwa ni Rais Hifipekunye Pohamba anawania muhula wa pili baada ya ushindi wqa kishindo katika uchaguzi wa mwaka 2004.

Kiongozi wa upinzani, Hidipo Hamutenya, aliyejitenga kutoka Swapo mnamo mwaka 2004 anatarajiwa kumsumbuwa Bw.Pohamba katika uchaguzi utakaofanyika kwa siku mbili

No comments:

Post a Comment