KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, November 27, 2009

Mkuu wa majeshi Ujerumani aachia ngazi


Jenerali wa Ujerumani amejiuzulu kufwatia mashambulio ya angani ya vikosi vya kujihami vya Nato ambapo raia waliuawa, waziri wa ulinzi amesema.
Wolfgang Schneiderhan amejiuzulu kutokana na shambulio la Septemba 4 eneo la Kunduz.

Uamuzi wake umetokana na ripoti kuwa taarifa kuhusu shambulio hilo-liloamrishwa na kamanda wa Ujerumani - hazikuwekwa wazi, waziri wa ulinzi alisema.

Inasemakana kuwa shambulio hilo liliwauwa raia wengi waliokuwa wakichota mafuta.

Wapiganaji wa Taliban waliteka magari mawili ya mafuta yakitoka Tajikistan kuelekea Kabul yakiwa na bidhaa za vikosi vya Nato.

Idadi ya raia waliouawa haijulikani.

No comments:

Post a Comment