KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, November 27, 2009

Mahujaji leo waingia katika bonde la Arafa


Zaidi ya mahujaji millioni mbili wamewasili katika nyanda za Arafat katika siku ya pili ya ibada ya Hijjah.
Mvua kubwa ya mawe iliyoambatana na dhoruba kali ilinyesha mwanzoni mwa ibada hii takatifu siku ya Jumanne na kusababisha uharibifu katika maeneo matakatifu na vifo vya takriban watu 44.

Lakini hali ya hewa inaonekana kutulia na mamilioni ya mahujaji wamekusanyika katika nyanda za Arafat. Kwa mahujaji wengi huu ni wakati wa msisimko mkubwa unaozingatiwa kuwa ni kilele cha hijjah takatifu.

Hapa ndipo mtume Muhammad(SAW) alisimama karne 14 zilizopita na kutoa hotuba yake ya mwisho.Tangu wakati huo kila mwaka waislamu wamekuwa wakikusanyika hapo kusali na kuomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu

No comments:

Post a Comment