KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, November 27, 2009

Panga kumkosakosa Benitez


Mkurugenzi mkuu wa Liverpool Christian Purslow amesisitiza nafasi ya Rafael Benitez ni madhubuti, licha ya kutolewa ligi ya mabingwa wa Ulaya.
Liverpool imeshindwa kusonga mbele hatua ya makundi kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka sita, licha ya ushindi kuifunga Debrecen bao 1-0.


Lakini Purslow amesema Benitez ataendelea kufundisha na akaongeza: "Hayupo hatarini.

Amesisitiza kwamba Benitez amesaini mkataba mpya wa miaka mitano na ndio kwanza amemaliza miezi minne chini ya mkataba huo, kwa hiyo kuujadili mkataba wake sio sahihi.

No comments:

Post a Comment