KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, November 27, 2009

Avram Grant ateuliwa kuifunza Portsmouth


Aliyekuwa kocha wa klabu ya Chelsea hapo zamani, Avram Grant, ametangazwa kuwa meneja wa Portsmouth baada ya Paul Hart kutimuliwa kufuatia kiwango cha timu hiyo kuzidi kuzorota.
Hii ni mara ya pili kwa Grant kufanya kazi kwenye klabu hiyo, mara ya kwanza alitumika chini ya Harry Redknap ambaye sasa yuko na Tottenham.

Raia huyo wa Israili aliwahi kushika wadhifa kama huo wa mkurugenzi mtendaji wa soka wa klabu ya Chelsea kabla ya Mourinho kutimuliwa na yeye kuteuliwa kama kocha.

Grant ataanza kwa mchuano utakaotangazwa na ''Ulimwengu wa Sokar'' Jumamosi hii kati ya Portsmouth na Manchester United.

No comments:

Post a Comment