KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Wednesday, November 25, 2009

Al Shabab lashutumu shirika la WFP




Moja ya makundi ya wapiganaji nchini Somalia limesema kwamba msaada wa chakula unaotolewa na Umoja wa Mataifa umezorotesha kilimo nchini humo.
Katika taarifa wapiganaji wa Al Shabab ambao sasa wanadhibiti sehemu kubwa ya kusini mwa Somalia wanalishutumu shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP kwa kuhujumu juhudi za wasomali za kuzalisha chakula chao wenyewe.



Kundi hilo la Al Shabab linataka Umoja wa Mataifa kuacha kuagiza chakula kutoka nje na badala yake kununua chakula kutoka wakulima wa Somalia. Shirika hilo la mpango wa chakula halijasema lolote kuhusu taarifa hiyo ya Al Shabab

No comments:

Post a Comment