KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, November 27, 2009

Mshukiwa wa mauaji nchini Ufilipino ajisalimisha


Mtu mmoja maarufu huko Ufilipino ambaye anatoka ukoo wa Ampatuan amejisalimisha kwa maafisa wanaochunguza mauaji yaliofanyika mapema wiki hii.
Andal Ampatuan Junior, ambaye ni Meya katika eneo la kusini mwa kisiwa cha Mindanao, alisafirishwa kwa helkopta ya kijeshi hadi katika mji mkuu wa Manila na kwa sasa anafanyiwa uchunguzi.

Bw. Ampatuan amekanusha kushambulia familia ya mpinzani wake wa kisiasa, ambapo watu wasiopungua 57 waliuawa.

Ukoo wa Ampatuan kwa miaka mingi umekuwa ukimuunga mkono rais Gloria Arroyo.

No comments:

Post a Comment