KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, November 27, 2009

Mke wa Berlusconi adai mamilioni


Aliyekuwa Mke wa Waziri Mkuu wa Italy Silvio Berlusconi amewasilisha madai ya kutaka alipwe fidia ya kuachika ya euro milioni 43, kwa mujibu wa taarifa za vyombo vya habari.
Veronica Lario aliwasilisha ombi la kuachika mnamo mwezi May, baada ya kuchukizwa na tetesi za mumewe kutoka na binti mwenye umri mdogo wa miaka 18.

Gazeti la Corriere della Sera la nchini Italia linasema kuwa Bw. Berlusconi amekubali kumpa Bi Lario, aliyezaa naye watoto watatu euro laki mbili kwa kila mwezi.

Duru zilizo karibu na kiongozi huyo zinasema kuwa takriban euro milioni 60 hadi sabini zimeisha kabidhiwa kwa Bi Veronica Lario. Bi Lario mwenye umri wa miaka 52 aliolewa na Bw.Berlusconi mnamo mwaka 1990 miaka kumi baada ya kukutana naye.

No comments:

Post a Comment