KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, November 9, 2009

Al Qaeda hawapo tena Afghanistan




Mkuu wa majeshi ya Uingereza, Sir Jock Stirrup, ameielezea BBC kwamba kundi la kigaidi la Al Qaeda haliendeshi tena oparesheni zake kutoka Afghanistan.

Alisema wapiganaji wachache wa kundi hilo sasa wanapatikana katika eneo dogo la Pakistan.

Lakini Sir Jock amesisitiza kwamba ni oparesheni zinazoendelea nchini Afghanistan ambalo zimefanikiwa katika kuliangamiza kundi la Al Qaeda.




Waziri wa ulinzi wa Uingereza, Bob Ainsworth, ameonya kwamba Marekani italazimika kufanya uamuzi wa haraka kuhusu mbinu zake nchini Afghanistan, hasa kama mataifa wanachama wa muungano wa NATO yangelipenda kutekeleza mipango yake na kupata ufanisi haraka

No comments:

Post a Comment