KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, October 20, 2009

Waamuzi wafungiwa maisha Tanzania


Waamuzi wafungiwa maisha Tanzania

Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF, limewafungia maisha waamuzi wanne wa soka, kuchezesha mchezo huo kutokana na tuhuma za rushwa.
TFF imewataja waamuzi hao kuwa ni Osman Kazi, Omar Miyala, Omar Mfaume na Kamwanga Tambwe.

Wakati huohuo kampuni inayoendesha soka nchini Kenya, KFL imesema wakurugenzi wake watakutana wiki hii, kujadili hatua watakayochukua dhidi ya kocha wa timu ya taifa ya nchi hiyo Harambee Stars.

KFL inataka kumchukulia hatua kwa tuhuma za utovu wa nidhamu na matokeo mabovu ya Stars.

No comments:

Post a Comment