KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Tuesday, October 20, 2009

Kocha wa Afrika Kusini ajiuzulu

Kocha wa Afrika Kusini ajiuzulu

Kocha mkuu wa timu ya soka ya Afrika Kusini Joel Santana, amejiuzulu kazi yake, ikiwa ni miezi minane kabla ya kuanza kwa michuano ya Kombe la Dunia.
Timu hiyo imepoteza michezo yake minane kati ya tisa iliyocheza.


Kuondoka kwa Santana kulikuwa kukitarajiwa, baada ya timu hiyo kupoteza michezo miwili ya kirafiki wiki iliyopita dhidi ya timu za taifa za Norway na Iceland.


Joel santana, mwenye umri wa miaka 60, ni kocha wa 15 wa Afrika Kusini, na aliteuliwa kukiongoza kikosi hicho mwezi April mwaka 2008, baada ya Carlos Parreira kujiuzulu kufuatia sababu za kifamilia.

Hata hivyo kuna tetesi kuwa Parreira huenda akarejea

No comments:

Post a Comment