KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, August 6, 2011

Mwandishi wa BBC awekwa kizuizini Misri





Shaimaa Khalil
Mwandishi wa BBC, Shaimaa Khalil, aliyekamatwa katika eneo la wazi la Tahrir kwenye mji mkuu wa Misri, Cairo ameachiwa huru.

Mazingira yake ya kuwekwa kizuizini siku ya Jumatatu mpaka sasa haiko wazi, lakini ilitokea baada ya wanajeshi, walioungwa mkono na polisi walipokwenda kwenye eneo walipokusanyika watu wengi kwa wiki tatu.

Walioshuhudia wameliambia shirika la habari la AFP kuwa waandamanaji walipigwa na simu zao za mkononi kuvunjwa.

Walisema, mtu yeyote aliyeonekana kupiga picha alishambuliwa.

BBC imetoa wito kwa mamlaka ya nchi hiyo kumwachia Khalil haraka iwezekanavyo.

Shirika hilo limesema katika taarifa yake, " Tuna wasiwasi sana juu ya kuwekwa kizuizini kwa Shaimaa Khalil huko Cairo. Ni mwandishi mzuri wa habari, akifanya tu kazi yake. Tunafanya kila liwezekanalo ili aachiwe."

No comments:

Post a Comment