KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, July 2, 2011

Gavana wa Hama, Syria, afukuzwa kazini



Rais Assad wa Syria amemtoa kazini gavana wa mji wa Hama, siku moja baada ya kufanywa maandamano makubwa mengine huko dhidi ya serikali yake.



Kufukuzwa kwa gavana huyo kulitangazwa kwenye televisheni ya taifa.

Hapo jana iliarifiwa kuwa watu kama nusu milioni waliandamana katika mji wa Hama, bila ya kuzuwiliwa na askari wa usalama.

Mkaazi mmoja wa mji alisema Hama ni eneo lilokombolewa.

Mji huo ni kati ya mizizi ya maandamano nchini Syria, ambayo sasa yameendelea kwa miezi mine.









Strauss-Khan aachiwa bila dhamana





Aliyekuwa mkuu wa shirika la fedha duniani, IMF Dominique Strauss-Khan ameachiwa huru baada ya kupewa kifungo cha nyumbani na kurejeshewa dhamana yake ya dola za kimarekani milioni 3.7.

Imeripotiwa waendesha mashtaka wamekubaliana kuwa Bw Strauss-Khan aachiliwe huru "kwa udhamini wake mwenyewe," ikimaanisha aahidi kufika mahakamani.

Anatuhumiwa kumdhalilisha kijinsia mhudumu kwenye hoteli moja mjini New York mwezi Mei 14.


Bw Strauss-Khan na mkewe


Lakini kesi hiyo inakaribia kufutwa baada ya kuibuka mashaka makubwa juu ya uaminifu wa aliyemshtaki.

Mwanasiasa huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 62 - aliyeonekana kuwa miongoni mwa wagombea wa urais wanaoongoza- alifika mahakamani siku ya Ijumaa.

Baada ya kutathmini taarifa za mwendesha mashtaka kutoka kwenye ofisi ya mahakama ya wilaya ya Manhattan, jaji ametangua masharti makali ya dhamana aliyopewa na Bw Staruss-Khan, lakini aliamuru kushikiliwa kwa hati yake ya kusafiria ili asiweze kusafiri nje ya Marekani.

Miongoni mwa yaliyowasilishwa ni taarifa kuwa mhudumu huyo alitoa ushahidi usio wa kweli kwa wazee wa baraza, bila kusema alisafisha chumba chengine kabla ya kumwambia msimamizi wake juu ya madai ya kudhalilishwa kijinsia.











Tanzania kuanza kuchimba madini ya Urani






Duma wa Selou
Tanzania itaanza kuchimba madini ya urani katika mbuga ya wanyama ya Selous, eneo lililo chini ya udhamini wa shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughilikia mazingira maarufu kama World Heritage.

Akizungumza na Idd Seif wa Idhaa ya kiswahili ya BBC, Waziri wa maliasili na utali iwa Tanzania, Ezekiel Maige, alisema kuwa sehemu wanayohitaji kutumia kwa kuchimbia mgodi wa urani ni 0.69%,

hivyo kupunguza eneo la mbuga ya wanyama kwa chini ya 1%.

Kwa mujibu wa Waziri Maige, WHC imesema itatoa kibali iwapo tu masharti ya kutunza mazingira yatakuwa yamezingatiwa. Fedha zitakazopatikana kutokana na madini hayo zitasaidia kutunza

mbuga hiyo alisema Maige.

Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Utamaduni UNESCO, hekta milioni tano la hifadhi ya mbuga ya Selou ina idadi kubwa ya Tembo, vifaru weusi, Chita, viboko na mamba na haijaharibu na

shughuli zozote za kibinadamu.

Katika mahojiano na Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Bw Maige alisema mradi huo bado uko katika hatua za mwanzo lakini utaathiri kwa asilimia 0.69 tu ya mbuga ya sasa na utakuwa ni chanzo muhimu

cha mapato ya nchi.

Makampuni yanatarajia kupata $200 milioni kwa mwaka kutokana na uchimbaji wa Urani na kati ya hizo $5 milioni zitalipwa kwa serikali ya Tanzania, alisema.

Sehemu ya mapato hayo itasaidia kutunza mbuga hiyo na mradi utatoa ajira kwa watanzania 1,600.

Katika mkutano wa mwaka wa kamati ya WHC, waziri Maige alisema, kulikuwa pia na wasiwasi kuhusu Msitu wa hifadhiwa Undendeule ulio kusini mwa mbuga ya Selou.

Lakini Bw Maige ambaye pia anashughulikia Utalii alisisitiza kuwa hakutakuwa na mathara kwenye msitu huo wa hifadhi ambao kwa sasa unaigharimu serikali $490,000 kwa mwaka kuutunza. Na

mapato yatakayotokana na uchimbaji wa madini hayo utasaidia kulipa askari wanaodhibiti ujangili.

Alisema Tanzania haikuhitaji kibali kutoka UNESCO ili kuendelea na mpango wake wa kuchimba Urani, lakini mataifa ya Afrika Mashariki yalitaka kujiridhisha na mapendekezo ya shirika hilo.

"mradi huu wa Urani utaanza," aliiambia BBC.

Aliongeza kuwa WHC Tanzania ifanye tathmini yenyewe itakayopitishwa na Tume ya Mazingira ya nchi hiyo.

Hatua ya pili ilikuwa ni hitaji la ujumbe wa wataalam kutoka UN kutembelea aeneo hilo na kutoa mapendekezo yake kuhusu kulinda na kutunza mfumo wa ekolojia.

Waziri alisema baada ya uamuzi huu taarifa itapelekwa katika mkutano mwingine wa WHC mwakani kuhusu mipaka ya Mbuga ya Hifadhi ya Selou.

Bw Maige aliongeza kuwa utafiti unaonyesha kuwa hakuna haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu sumu ya mionzi inayotokana na uchimbaji wa Urani katika eneo hilo.

"Kiwango cha mionzi kitabakia kuwa kile kile, haitakuwa na hatari kwa binadamu," alisema.








Murray aondolewa na Nadal



Bingwa mtetezi wa mashindano ya Wimbledon yanayofanyika nchini Uingereza, Rafa Nadal amemshinda Muingereza Andy Murray na kuzima ndoto ya Waingereza kumpata bingwa Muingereza wa kwanza katika kipindi cha miaka 75.



Tumaini la Uingereza


Nadal amemshinda Murray kwa kipigo cha uhakika kwa seti tatu kwa moja baada ya Andy Murray kuwapa matumaini mashabiki wake waliofurika uwanja wa kati ya Wimbledon akiondoka na ushindi wa 7-5.

Baada ya seti hiyo Murray aliendelea hivyo hadi mchezo wa tatu Nadal alipoanza kutoa makucha yake na kubadili mchezo hatimaye akishinda 6-2, 6-2, 6-4.


Rafael Nadal


Nadal ambaye hadi wakati huu alikuwa namba moja atapambana na Novak Djokovic ambaye alifuzu kwa fainali inayochezwa siku ya jumapili kumpata bingwa wa mwaka huu.


Novak Djokovic



Jo Wilfred Tsonga
Licha ya kushinda nusu fainali ya kwanza, Novak Djokovic kutoka Serbia alipewa kibarua na Mfaransa Jo-Wilfred Tsonga ambaye babake alitoka Jamhuri ya Congo.

Andy Murray alijitahidi katika mchezo huu lakini maarifa na utayarifu wa Nadal ulimzidi na kudhihirisha tofauti baina ya mwanafunzi na mwalimu.

Nadal ambaye wiki ijayo atapoteza nafasi yake ya kuwa mchezaji bora duniani kwa Novak Djokovic ameonyesha nia ya moyo wa kutaka kushinda mashindano haya tangu mwanzo.

Djokovic atatangazwa mchezaji namba moja duniani wiki ijayo kutokana na kufululiza kushinda mashindano mengi aliyoshiriki mwaka huu.










Morocco wapiga kura mabadiliko ya Mfalme







Mfalme wa Morocco Mohammed VI aliingia madarakani 1999

Wananchi wa Morocco wanapiga kura katika mfululizo wa mageuzi na mabadiliko ya kikatiba.

Mapendekezo hayo yaliletwa na Mfalme Mohammed VI na yanalenga kumpa waziri mkuu na bunge mamlaka zaidi.

Wachambuzi wanasema anatarajiwa kushinda japokuwa kujitokeza kwa wachache kunaweza kuamsha madai ya mabadiliko zaidi..

Mabadiliko yake yamechochewa na maandamano yanayoendelea katika nchi za kiarabu ambayo yaliyowaondoa madarakani marais wa Tunisia na Misri.

Vijana wa Morocco waliandaa vuguvugu lao kupitia mitandao ya kijamii mwezi Februari kwa wiki kadhaa kutaka kuwepo mabadiliko imbayo hatua iliyowafanya maelfu ya watu kuingia mitaani. Wamewataka wafuasi wao kususia kura hiyo.

"Tunakataa kilichopendekezwa. Bado kinawaacha vinara katika sehemu," mmoja wa waratibu wa vuguvugu hilo Najib Chawki aliliambia shirika la habari la Reuters

Baadhi wanaiita ‘siku kubwa ya maamuzi’ nchini Morocco. Hata hivyo wamorocco wanaonekana kuendelea na maisha yao ya kila siku bila vurugu yoyote ikilinganishwa na wakati wa rasimu ya mabadiliko. Baadhi ya watu wanasema in ukimya tu klabla ya mshindo mkuu.

Katika moja ya vituo vya kupigia kura katika eneo la Shule ya Hassan II katika mji mkuu Rabat, vyumba vyote vya kupigia kura vilikuwa sawa. Vina bendera ya Morocco na picha ya mfalme,

vyote vikiwavimewekwa pamoja katika ubao wa kufundishia. Ushiriki ulikuwa wa taratibu asubuhi lakini watu wanasema wengi watajitokeza baada ya swala ya Ijumaa.

Kuna dalili za matarajio katika ufalme, watu wengi wanahisi kuwa wanaandika historia na pia watu wanapiga kura kwa makini sana. Wanajua kuwa kura yao iwe –ndiyo au hapana- inaweza kuwakiliosha rasimu kwa mfalme mwenyewe.

Lakini vyama vyote vikuu vya upinzani, vyama vya wafanyakazi, vikundi vya kiraia na viongozi wa kidini na vyombo vya habari a kwa wiki kadhaa sasa vimekuwa vikiwataka wamorocco kupiga kura kuunga mkono katiba mpya.

Kura hiyo inayowakilisha rasimu ya mabadiliko ya kwanza ya katiba chini ya utawala wa mfame wa miaka 12, imeelezwa kuwa ‘tarehe ya kihistoria.’







Urusi: Wafaransa wamekuka maadili Libya



Waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov amelaani hatua ya Ufaransa kuwapa silaha waasi wanopinga utwala wa kanali Muammar Gaddafi.

Bw Lavrov anasema hatua hio ikiwa imedhibitshwa ni kosa kubwa kwani imekiuka azimio 1970 la umoja wa mataifa ambalo linazuia silaha kuingizwa nchini humo na pande zote husika kwenye mzozo huo.



Operesheni ya NATO Libya


Wanjeshi wa Ufaransa walikiri kuwaangushia silaha wapiganaji wa kabila la Berber wanaoishi kwenye maeneo ya milima kusini mwa mji mkuu wa Tripoli.

Umoja wa Afrika pia umelaani uaamuzi wa Ufaransa wa kuimarisha nguvu za kijeshi za waasi hao.

Mwenyekiti wa tume ya Umoja huo Jean Ping amesema kitendo hicho kinaweka eneo zima hatarini.

Waziri wa mambo ya nje wa urusi amepanga kukutana na mwenzake kutoka Ufaransa Alain Juppe mjini Moscow kudhibitisha suala hilo tete.

Serikali ya urusi ilisusia kupigia kura mswada uliowasilishwa kwenye baraza la usalama la umoja wa mataifa kuruhusu harakati za kijeshi nchini Libya.

Mzozo unaoendelea mjini Libya ndio umepewa kipa umbele katika mkutano wa viongozi wa Afrika unaoendelea nchini Equatorial Guinea.

Bw Ping amesema kuna uwezekano mkubwa vita vya wenyewe kwa wenyewe vikazuka nchini humo sawa na hali iliyoko nchini Somalia.

Mwenyekiti wa tume hiyo ya Umoja wa Afrika amefahamisha BBC kuwa mpango wa amani uliyobuniwa mnamo mwezi March bado unazingatiwa.

Mpango huo unataka pande zote zisitishe mapigano ili mazungumzo ya amani yaweze kuanza.

Habari kwamba Ufaransa imedondosha silaha nchini Libya zilijitokeza kupitia gazeti la Ufaransa, Le Figaro la jumatano.

Gazeti hilo lilisema kuwa Ufaransa, nchi inayoongoza operesheni ya NATO nchini Libya haikufahamisha nchi wanachama wenzake kuhusu operesheni hio.

Uwamuzi huo ulifikiwa baada ya mkutano uliofanyika mwezi April kati ya Rais Nicolas Sarkozy na Mkuu wa vikosi vya waasi wa Libya Gen Abdelfatah Younis.








India mbioni kudhibiti idadi ya watu






Ongezeko kubwa la idadi ya watu nchini India imewalazimu maafisa wa Afya kuanza kampeni mpya ya mpango wa uzazi.


Serikali inawasiwasi kuhusu idadi kubwa ya watu
Mpango huo mpya wa uzazi unanuia kuwashawishi wanawake na wanaume kukubali njia ya kumaliza kabisa nguvu za mayai ya uzazi.

Wanaokubali watapokea zawadi ya gari lipya miongoni mwa zawadi nyingine.

Tata nano, ndio gari lenya bei rahisi sana duniani lakini kulingana na kampeni hiyo, bila shaka kuna uwezekano likawa maarufu zaidi nchini India katika siku chache zijazo.

Dakatri Sitaram Sharma anatazamia kuwa huenda gari hilo likawa kishawishi tosha kwa wakazi wa jimbo la Jhunjunu kujitokeza kufungwa kizazi.

Lengo la Daktari Sharma ni kuwa jumla ya wanawake na wanaume elfu 20 watajitokeza kufungwa kizazi.

Kwa taarifa yako, gari sio zawadi tu itakayotolewa kwenye kampeni hiyo. Watakao fika watapewa piki piki, televisheni na vifaa vya kisasa vya kusagia vyakula.

Mpango huo hauja lenga tuu wakaazi wa jimbo hilo ambalo mara nyingi linakabiliwa na ukame.

Serikali ya India imekuwa ikitatizika na idadi ya raia wake ambayo inakuwa kwa kasi sana.

Hofu za utawala nchini India ni kuwa ifikiapo mwaka wa 2030, heunda idadi ya watu walioko nchini humo ikazidi ile ya wachina.

Hata hivyo hakuna uhakika kuwa kampeni hii itaungwa mkono kote nchini India.

Mwaka wa 70 ilipojaribiwa, maelfu ya watu walijotekeza kisha serikali ikashindwa kutimiza ahadi zake kitu kilicho wachukiza wengi ambao walidai kuwa serikali ilikuwa imewalaghai.







Sudan kuondoa majeshi kabla ya uhuru




Rais wa Sudan Omar al-Bashir na Kiongozi wa Sudan Kusini Salva Kiir

Majeshi ya pande zinazozozana nchini Sudan yamekubaliana kuondoka katika mpaka wa kaskazini kusini, kabla ya uhuru wa Sudan wiki ijayo.

Makubaliano hayo yaliyofikiwa Ethiopia yamekuja baada ya mapigano katika mipaka miwili ya maeneo ya Abyei na Kordofan Kusini, yaliyowalazimu watu wapatao 170,000 kukimbia makazi yao.

Majeshi hayo yakiondoka yatatakiwa kuacha sehemu yenye umbali wa kilometa 20 (maili 12) kutoka eneo la mapambano.

Mapigano hayo yamezusha hofu kuwa miaka 21 ya vita vya Kusini na Kaskazini vinaweza kuanza tena.

Makubaliano hayo yaliyofanyika chini ya uongozi wa Rais wa zamani wa Afrika Kusini Thabo Mbeki yanafuatia mengine kadhaa yalimaliza mapigano ya Abyei na Kordofan Kusini.

Waangalizi wa Kimataifa na vikosi vya kulinda amani vya UN vitasimamia makubaliano hayo.

Pande zote mbili zinaing'ang'ania Abyei; wakati mapigano ya Kordofan Kusini yanatokana na vikosi vya kaskazini kupigana dhidi ya kabila la Wanuba waliowasaidia waasi wa Kusini wakati wa vita vya

wenyewe kwa wenyewe lakini kwa sasa wamejikuta wakiwa upande wa Kaskazini.

Mwandishi wa BBC Peter Martell aliyeko mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba anasema makubaliano hayo si rahisi yakatekelezwa kama inavyosikika kwa sababu maeneo hayo bado yanagombewa na mipaka bado haijatengwa.

Anasema makubaliano haya yataleta faraja kwa wengi Juba lakini watakuwa makini kuhakikisha kuwa yanatekelezwa.

Jumanne ilikubaliwa kuwa wapiganaji wa zamani wa Sudan Kusini walioko Kordofan Kusini watatakiwa kujiunga na jeshi la Kaskazini au wanyang’anywe silaha.

Makubaliano hayo yaliyosimamiwa na Umoja wa Afrika yanahusisha pia jimbo jirani la Blue Nile ambalo lina wapiganaji wa zamani wa kusini. Hata hivyo limekuwa halina mgogoro wowote.

Makubalino yanataka pia kuwa zoezi la kuwanyang’anya silaha lisitumie nguvu.

Mapema wiki hii Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa lilipitisha azimio la kupeleka vikosi 4,200 vya kulinda amani kutoka Ethipia katika eneo la Abyei baada ya makubaliano ya awali kulifanya lisiwe eneo la vita.

Pande hizo mbili bado hazijafikia muafaka namna zitakavyogawana utajiri wa mafuta baada ya Uhuru.

Asilimia 75% ya eneo la mafuta iko upande wa Kusini lakini mabomba ya mafuta yanaelekea kaskazini mpaka eneo la Bandari katika bandari ya Port Sudan iliyoko pwani ya bahari ya Shamu.

Kwa sasa mapatao yanatakiwa kugawanywa sawa kwa pande zote mbili.








Bunge lapitisha mswada muhimu Ugiriki




Makabiliano makali kati ya polisi na waandamanaji wanaopinga mpango wa kuunusuru uchumi wa Ugiriki yameendelea mjini Athens kutwa nzima.


Raia wanapinga mpango huo ambapo kodi itaongezeka maradufu
Mabomu yaliotengenezwa na petroli yamekua yakilipukua jioni nzima, huku polisi wakutuliza ghasia wakiwarushia watu hao waliokusanyika nje ya jengo la bunge gesi za kutoa machozi.

Lakini licha ya vurugu hizo, mswada wa serikali uliochochea machungu haya yote ulipitishwa japo katika mazingira ya ushindani mkali.

Wabunge 155 waliunga mkono pendekezo hilo huku wengine 138 wakipinga. Leo wabunge watapiga kura tena kubadilisha sheria ili mpango huo utekelezwe.

Waziri mkuu George Papandreou amelenga kubana matumizi ya serikali ili ifikiapo mwaka wa 2015 watakuwa na hazina ya pauni bilioni 25.

Pamoja na hilo, amependekeza kupandisha kodi ili kuongezea kipato cha serikali, hatua iliochochea maandamano hayo nchini humo.

Lakini waziri mkuu Papandreou anasema mpango huo ukitibuka ni sawa na kuangamiza nchi hiyo.

Umoja wa ulaya umepongeza bunge kupitisha pendekezo hilo ambapo liki zingatiwa serikali ya Ugiri huenda ikafaulu kulipa malimbikizi ya madeni yake.

Hata hivyo bado kuna wale ambao hawaamini kuwa mpango huo utafaulu.

Serikali ya Ugiriki sasa inatarajia kupata mkopo wa euro billioni 110 kutoka kwa shirika la fedha duniani na umoja wa ulaya kutatua matatizo yake ya kiuchumi.







Radi yasababisha vifo zaidi Uganda



Nchini Uganda radi imesababisha vifo vya wanafunzi 18 na wengine 50 kujeruhiwa ilipopiga shule moja ya msingi magharibi mwa nchi hiyo.


Ramani ya Uganda

Msemaji wa polisi Judith Nabakooba ameliambia shirika la habari la AFP kuwa wanafunzi wakike 15 na wakiume watatu walikufa jana jioni katika shule ya msingi ya Runyanya wilaya ya Kiryandongo.

Wasiwasi kuhusu mfululizo wa radi kali zinazoipiga Uganda kwa wakati huu umesababisha wabunge nchini humo kulijadili suala hili bungeni.

Wasiwasi

Wiki iliyopita watu wasiopungua 28 waliuawa na radi na wengine kadhaa kujeruhiwa.

Kwa mujibu wa mwanasayansi anayeshughulika na masuala ya hali ya hewa kutoka Uganda Kiza Aderi, ukosefu wa vifaa vya kukabiliana na radi katika majengo kadhaa huenda ikiwa ni moja wapo ya sababu zinazosababisha watu kuuawa na radi.

Kamanda wa polisi wa wilaya ya Kiryandongo Patrick Byaruhanga ameliambia gazeti la taifa la New Vision kuwa radi hiyo ilipiga karibu saa kumi unusu jioni za Uganda wakati wanafunzi walikuwa bado madarasani wakisubiri mvua itue kabla ya kwenda nyumbani.

Msemaji wa polisi amesema baadhi ya waliopata majeraha makubwa wamepelekwa katika hospitali ya Mulago katika mji mkuu wa Kampala kilomita 200 kusini mashariki ya Uganda.

Nchi ya Uganda inashuhudia kipindi cha mvua na dhoruba kali na visa vya vifo kutokana na radi vimewatia watu wengi wasiwasi.










Ufaransa imewapa waasi wa Libya silaha



Muasi wa Libya


Ufaransa imewarushia silaha waasi wanaopigana na majeshi ya Kanali Gaddafi magharibi mwa Libya, jeshi la Ufaransa limethibitisha.

Silaha na risasi zilipelekwa kwa wapiganaji wa kikabila wa Berber katika milima ya Nafusa.

Awali, ripoti iliyotolewa na gazeti la Le Figaro lilisema silaha hizo ni pamoja na roketi na makombora.

Ufaransa, nchi inayoongoza harakati za kijeshi za umoja wa nchi za kujihami za Ulaya Nato, haikuwaeleza washirika wao kuhusu hatua hiyo, limesema gazeti la Le Figaro.

Msemaji wa jeshi la Ufaransa, Kanali Thierry Burkhard alisema, " Tulianza kwa kurusha msaada wa kibanadamu: chakula, maji na vifaa vya matibabu".

Aliliambia shirika la habari la AFP, " Wakatai wa harakati hizi, hali ya raia ilizidi kuwa mbaya. Tuliwarushia silaha na vifaa vya kujilinda, hasa risasi.









Nigeria yapata vichochea uchumi




Banki ya ujasiriamali ya Morgan Stanley, imetabiri kuwa uchumi wa Nigeria itakua kwa haraka katika kipindi cha kati, na kuupita ule wa Afrika Kusini ifikapo mwaka 2025 na kuwa yenye uchumi mkubwa zaidi barani Afrika. Utabiri huo unakuja wakati uchumi wa Afrika nzima ukianza kuongezeka kwa haraka.

Taarifa ya Morgan Stanley iliyopewa jina 'Uchumi wa Nigeria wapata nguvu ya kuimarika' - inatoa mwangaza kuhusu majaliwa ya nchi hiyo. Taarifa hiyo inatabiri kukuwa kwa asili mia 8 katika kipindi cha miaka miwili ijayo.



Rais Goodluck Jonathan


Hali hii, kama inavyosema Benki hiyo, imesababishwa na mambo kadhaa. Muhimu na siyo la kustaajabisha ni bei ya mafuta. Lakini kuna vichochezi vingine pia.


Umeme waimarishwa
Kati ya hivi ni pamoja na nyongeza ya mishahara kuwaongezea kipato raia wenyewe pamoja na matumaini ya mashirika yanayotoa huduma ya nguvu ya umeme kufanikiwa kuondoa tatizo la umeme.

Benki hiyo inaelezea kuhusu athari za kuyumbayumba kisiasa, lakini kwa sasa hali ni shuari. Taarifa hiyo inatoka wakati gazeti la hapa Uingereza limenukuu Benki ya Uingereza ''Standard chartered bank'' ikitazamia ilichokiita mpasuko wa kukuwa kwa biashara baina ya bara Asia na Afrika katika kipindi cha miaka ishirini ijayo.

Wakati Nigeria na Mataifa mengine ya Kiafrika yakishika kasi ya maendeleo, Afrika kusini itaachwa nyuma,taarifa hiyo inatabiri.







Amri Nigeria kuhusu maeneo ya burudani



Mashambulizi ya bomu Nigeria


Serikali ya Nigeria imetoa amri na maagizo ya saa za kufungwa vilabu, baa na majumba ya cinema katika mji mkuu wa Abuja, hatua hii inakuja wiki mbili baada ya mji wa Abuja kushambuliwa kwa mabomu.

Maeneo haya ya burudani kwa sasa yatalazimika kufunga shughuli zake kufikia saa nne za usiku za Nigeria. Nayo mabostani ya umma yanayotembelewa na watoto, sasa yanapaswa kufunga milango yake saa kumi na mbili jioni.

Watu wanane walikufa katika mashambulizi ya hivi majuzi yaliolenga makao makuu ya Polisi. Mashambulizi hayo yalitekelezwa na kikundi cha wanamgambo wa Kiislamu wenye itikadi kali cha Boko Haram.

Kikundi hicho pia kinashutumiwa kwa mashambulizi ya Jumapili dhidi ya maskani moja ya wazi ya kunywa pombe katika eneo la Maiduguri.

Kikundi hicho ambacho kawaida hushambulia na hasa kulilenga jimbo la kaskazini mashariki la Borno kinasema kinapigania utawala wa Kiislamu na kinafanya kampeini dhidi ya shughuli zote za kisiasa na kijamii zilizo na uhusiano ama mvuto wa kimagharibi.










Simba yaunguruma Kagame





Timu ya Etincelles ya Rwanda imekuwa ya kwanza kuyaaga mashindano ya CECAFA Klabu Bigwa Afrika Mashariki na Kati maarufu kama Kombe la Kagame baada ya kufungwa kwa mara ya tatu mfululizo pale ilipofungwa na Red Sea ya Eritrea jumla ya magoli 4 – 1 katika mchezo wa awali ulifanyika katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Tanzania.

Katika mechi ya awali Etincelles ilifungwa na Zanzibar Ocean View 3-2 na baadae ikafungwa na Vital’o ya Burundi magoli 3-1.

Katika mechi ya pili iliyochezwa katika uwanja huo huo wa Taifa mjini Dar es Salaam Simba ya Tanzania imepata ushindi wake wa kwanza baada ya kuifunga timu ya Ocean View ya Zanzibar goli 1-0

Goli pekee la Simba limefungwa na Amir Mrisho Maftah katika kipindi cha kwanza kwa shuti kali akiwa umbali wa mita 40 na kumshinda mlinda mlango wa Ocean view Abass Nassor Ali.

Kabla ya kufunga goli hilo Amiri Mrisho Maftah alikosa penati baada ya mshambuliaji wa Simba Mussa Hassan Mgosi kufanyiwa faulo katika kisanduku cha kumi na nane.

Hadi kipindi cha kwanza kinamalizika matokeo yalikuwa 1-0.

Kipindi cha pili timu zote ziliingia uwanjani kwa shauku ya ushindi ambapo zilishambuliana kwa zamu hata hivyo kukosekana kwa umakini wa washambuliaji wa Simba kulifawanya wakose magoli mengi hadi fulimbi ya mwisho matokeo yalikuwa ni yale yale 1-0.

Kwa matokeo hayo Ocean View ya Zanzibar inaendelea kushika nafasi ya Kwanza kwenye kundi A ikufuatiwa na Vital'o ya Burundi nafasi ya pili ikiwa na pointi 4 sawa na Simba iliyopo nafasi ya tatu, Red Sea ya Eritrea nafasi ya tano ikiwa na pointi 3 na Etincelles ya Rwanda ya mwisho ambayo hadi sasa haijapata pointi hata moja.

Bunamwaya Uganda itashuka dimbani kumenyana na timu El Mereikh ya Sudan siku ya Alhamisi katika mchezo wa awali utakaochezwa katika uwanja wa Dar es Salaam na baadae Yanga ya Tanzania itashuka dimbani kupambana na timu ya Elman ya Somalia katika mchezo wa pili wa kundi B .








Barabara ya vumbi tosha Serengeti




Mipango iliyojaa utata ya kujenga barabara ya lami katikati ya mbuga ya wanyama ya Serengeti na sasa baada ya ubishi na kuonywa kuwa mpango huo utaathiri mazingira na nyenzo za wanyama pori.


Thamani ya mazingira ni kubwa




Serikali ya Tanzania ilipanga barabara mbili yaani ya kutoka na inayoelekea kupitia mbuga hiyo kutoka ukingo wa Ziwa Victoria na pwani.

Lakini utafiti uliofanywa umeonyesha kuwa mpango huo utaathiri vikali hali ya wanyama kama vile nyumbu na punda milia, ambao misafara yao ya kuhama, jambo ambalo linaangaliwa kama maajabu ya maumbile Duniani.

Serikali sasa imethibitisha kuwa barabara hiyo haitoguswa na itabaki kuwa ya vumbi.

Katika barua kwa Kituo kinachoshughulikia Hifadhi ya Mazingira Duniani mjini Paris, Idara ya mali asili na Utalii nchini Tanzania imesema kuwa sehemu ya barabara hiyo yenye umbali wa kilomita 50 itaendelea kusimamiwa kwa ajili tu ya utalii na utawala.

Serikali kwa sasa inatathmini njia nyingine ingawa itakuwa ndefu kuweza kuwafikishia wananchi wake huduma kupitia kusini mwa mbuga hiyo ya wanyama.

Barabara hiyo itaepuka maeneo yenye thamani ya kuhifadhi mazingira na athari zinazoweza kufuata.



Serengeti




Mwaka jana, kundi la wataalamu walionya kua barabara iliyopendekezwa kupitia mbuga ya wanyama inaweza kupunguza idadi ya Nyumbu wanaokadiriwa kuwa milioni 1.3 kufikia 300,000.

Athari kwa wanyama pori, wataalamu hao walionya kuwa Uchumi utaathirika mno kutokana na kupungua kwa wanyama hao.

Wataalamu hao waliitaja mbuga ya wanyama ya Serengeti kama mfano wa kipekee wa hifadhi ya wanyama wanaohamahama.

Safari ya kuhama hama kwa wanyama hao kila mwaka hushiriki takriban wanyama milioni 1.5, wakiwemo nyumbu na punda milia.

Wakati wanyama hao wakisafiri, huacha vinyesi ardhini, ambavyo husaidia kurutubisha mimea, huku nyayo zao zikizuwia ukuaji wa kupindukia wa nyasi.

Mabadiliko ya aina yoyote katika hali kama hiyo, wataalamu hao wamesema kwenye ripoti yao kwa serikali ya Tanzania, yatasababisha kupungua kwa wanyama wanaotegemea nyumbu na punda milia kama chakula chao kama simba,chui na duma.




Simba



Hawa ni baadhi ya wanyama wanaovutia mno watalii.

Halikdhalika wataalamu hao wameonya kuwa barabara hiyo ingeweza kusababisha kubadilika kwa mimea na vilevile kusafirisha aina mbalimbali za magonjwa yasiyokuemo ndani ya mbuga.







United yathibitisha kumsajili De Gea





De Gea
Manchester United imethibitisha kumsajili kipa David de Gea kutoka Atletico Madrid kwa mkataba wa miaka mitano.

Kipa huyo anayechezea pia timu ya taifa ya Uhispania kwa vijana wa chini ya umri wa miaka 21, alifanyiwa vipimo vya afya siku ya Jumatatu, kukamilisha uhamisho wake unaodhaniwa kuwa wa pauni milioni 18.9.

"Najivunia sana, na niko tayari kuanza kucheza hapa," amesema De Gea akizungumza na kituo cha televisheni cha Manchester United, MUTV.

"Klabu kubwa kama Manchester United ikikufuata, bila shaka utafurahi sana. Niko makini kufanya niwezavyo kuonesha uwezo wangu." Ameongeza De Gea.

Kukamilika kwa mkataba huo kunamfanya De Gea kuwa kipa wa pili wa gharama zaidi, nyuma ya Gianluigi Buffon ambaye alinunuliwa na Juventus kwa pauni milioni 32.6 mwaka 2001.









Kilio cha Wakimbizi wa Burundi



Siku ya kimataifa ya wakimbizi duniani iliadhimishwa Jumatatu, ikiwa ni siku ya kuwakumbuka na kuwatambua zaidi ya watu milioni nne waliotapakaa sehemu mbali mbali duniani baada ya kupoteza makazi.



Mmmoja wa wakimbizi kutoka Burundi


Wakati wakimbizi kutoka nchi mbali mbali walioko katika Jamhuri ya Kidemkrasia ya Congo wakikusanyika mjini Kinshasa kupata mafunzo kuhusu haki zao, ilikuwa ni majonzi kwa wakimbizi kutoka Burundi ambao wamekuwa wakiishi Tanzania.

Kwenye kambi ya wakimbizi ya Mutabila iliyoko wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma, siku hiyo iliadhimishwa kwa ilani kutolewa kwa zaidi ya wakimbizi elfu 35 kutoka Burundi walioko katika kambi hiyo, kuwa lazima warejee nyumbani.

Hakuna usalama

Serikali ya Tanzania inataka kambi hiyo kufungwa ifikapo tarehe 31 Disemba mwaka huu, na kwa hivyo wakimbizi wametakiwa kuanza kujiandaa kurudishwa nyumbani kuanzia mwezi Septemba.

Hilo halibadiliki, kwa hivyo ni wakati wa familia kukaa kufikiria swala la kurejea, kinyume na hapo mtapata taabu nyie
Idd Mpoma
Lakini wakimbizi hao baadhi yao walioishi Tanzania kwa karibu miaka 40 wanapinga pendekezo la kuwarudisha nyumbani Burundi, wakisema usalama uliopo hauridhishi.

'' Hali iliyo dhahiri ni kuwa vyombo vya habari nchini kwetu vinatangaza kuwa hakuna usalama wa kutosha. Taarifa hizo hutufanya wakimbizi tuogope sana maana aliuwawa mwenzetu, na aliyeumwa na Nyoka akiona unyasi hushtuka.'' Alisema msemaji wa wakimbizi hao.


Kambi ya Mutabila ni ya mwisho kwa wakimbizi kutoka Burundi ambao wamekuwa wakiishi Tanzania, baada ya kambi zingine mkoani Kigoma kufungwa.

Wengi wa wakimbizi waliokimbia Burundi kutokana na machafuko ya mwaka wa 1972 wameshapata uraia wa Tanzania , lakini wale ambao hawakuweza kupata uraia, pamoja na wakimbizi wengine walioingia nchini humo baada ya vita mwaka 1993 walipelekwa katika kambi ya Mutabila kusubiri kurejeshwa nyumbani.


Kambi ya Mtabila


Mwakilishi wa serikali ya Tanzania Idd Mpoma alisema wakati huu lazima wakimbizi waondoke kuanzia Septemba.

'' Hilo halibadiliki, kwa hivyo ni wakati wa familia kukaa kufikiria swala la kurejea, kinyume na hapo mtapata taabu nyie.''

Kwaya ya wakimbizi hao ilitunga wimbo maalumu kuwataka viongozi wa Tanzania kuwaongeza muda na kuelewa kuwa hawakujiombea kuwa wakimbizi.

Warejee kwao

Jumla ya wakimbizi zaidi ya 600,000 kutoka Burundi waliomba tokea mwaka wa 1972.

Warundi laki moja na elfu sitini wa kambi ya Katumba na Mishamo mkoa wa Rukwa mwaka jana walipewa uraia wa Tanzania.

Lakini wakimbizi 35,000 waliosalia wanatakiwa warejee kwao Burundi.

Mvutano uliojitokeza baina ya wakimbizi ,serikali za Burundi na Tanzania pamoja na shirika la umoja wa mataifa linaloshughulikia wakimbizi UNHCR umeacha swala hili kwenye njia panda, kuhusu nini kitatokea kuanzia mwezi Septemba wakati kundi la kwanza la wakimbizi elfu kumi litatakiwa kusafirishwa hadi Burundi.





Nato wafaulu kudhibiti shambulio kabul



Yamkini watu kumi na wawili wamefariki baada ya washambuliaji wakujitoa mhanga kuvamia hoteli ya kifahari ya Intercontinental mjini Kabul, Afghanistan.


Wakuu wa mikoa walikuwa wanafanya mkutano wakati wa shambulio hilo
Baada ya makabiliano ya saa tano katika hoteli hiyo, hatimae wanajeshi wa Nato wakitumia helikopta walifaulu kuwauwa wanamgambo wanne ambao walikuwa wamepanda kwenye paa la hoteli hiyo.

Kulingana na msemaji wa jeshi la Nato kanali Tim James, wanamgambo hao walikuwa wamevalia fulana zilizokuwa na mabomu.

Hoteli hiyo ya Intercontinental ni maarufu sana miongoni mwa raia wa kigeni, lakini wote walikuwa salama hata baada ya shambulio hilo.

Kulingana na maafisa wa uslama wa serikali ya Afghanistan, wamshambuliaji sita walivamia hoteli hiyo lakini wote sasa wameuawa.

Viongozi wa kundi la wanamgambo wa Taleban wamedai kuhusika na shambulio hilo ambalo lilitokea wakati wageni wengi walikuwa wanapata chakula chao cha jioni.

Msemaji wa idara ya usalama wa ndani nchini humo Siddiq Siddiqi amesema waliouawa ni raia wa Afghanistan na watu wengine nane walijeruhiwa katika tukio hilo.

Wakuu wa usalama wanasema huenda wanamgambo hao walikuwa wamelenga kushambulia mkutano wa wakuu wa mikoa uliokuwa ukiendelea kwenye hoteli hiyo.

Hoteli ya Intercontinental ni maarufu kuwa na usalama mzuri zaidi nchini Afghanistan.

No comments:

Post a Comment