KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, April 21, 2011

.



Mpinzani Nigeria apinga matokeo


Hoteli iliyopigwa bomu Kaduna




Mpinzani mkuu katika uchaguzi wa urais Nigeria, Jenerali Muhammadu Buhari, amesema kulikuwa na hila iliofanywa kwenye uchaguzi wa Jumamosi.

Bw Buhari ambaye aliwahi kuwa mkuu wa majeshi aliiambia redio ya Marekani kuwa kuna maeneo upande wa kusini wenye wafuasi wake wengi hawakuruhusiwa kupiga kura.

Lakini alisema chama chake kitapinga matokeo kwa mujibu wa sheria na kusihi kuwepo kwa amani baada ya ghasia kuibuka upande wa kaskazini kufuatia Goodluck Jonathan, aliyetoka kusini, kushinda.

Shirika la msalaba mwekundu limesema watu 48,000 kwa sasa wamekimbia vurugu hizo.

Katika jimbo la Kaduna, vyanzo vya polisi vimeiambia BBC takriban watu 400 wamekamatwa wakihusishwa na mapigano hayo.

Mwandishi wa BBC Abdullahi Kaura Abubakar amesema kwa sasa hali imetulia kwenye mji wa Kaduna, ambapo mitaa imejaa maiti zilizochomwa moto na wengine wakachoma makanisa, vituo vya polisi pamoja na nyumba baada ya siku mbili za ghasia.

Alisema, mapigano yanaendelea katika maeneo mengine ya jimbo hilo na majeshi ya usalama yamesambazwa zaidi maeneo hayo.

Bw Jonathan alitangazwa kuwa mshindi kwenye uchaguzi wa rais siku ya Jumamosi, huku tume ya uchaguzi ikisema kapata takriban asilimia 57 ya kura zote ambayo ni kura milioni 22.5 ukilinganisha na kura milioni 12.2 za Bw Buhari.

Waangalizi wa kimataifa walisema uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki.










Waasi wakataa kuweka silaha chini Libya





Wapiganaji wa Waasi nchini Libya
Upinzani nchini Libya, umekataa pendekezo la hivi punde kutoka kwa serikali ya Kanali Muammar Gaddafi, la kuwataka kuweka silaha chini.

Msemaji wa baraza la mpito linalodhibiti mji wa Benghazi, amesema kuwa wapiganaji wa upinzani wataendelea na vita dhidi ya vikosi vya Kanali Gaddafi.

Msemaji wa kundi hilo la upinzani, Abdul Hafeel Ghoga, amewaambia waandishi wa habari kuwa Kanali Gaddafi, amependekeza mkataba huo wa kusitisha mapigano, kwa sababu wanajeshi wake wanaendelea kuangamizwa kwenye mashambulio ya anga yanayotekelezwa na wanajeshi wa NATO.

Lakini Bwana Ghoga, amesema upinzani hauwezi kusimamisha mashambulio yake dhidi ya wanajeshi wa serikali.

Akizungumzia pendekezo la kuafikiwa kwa mkataba wa kisiasa ambao utaruhusu kiongozi wa Libya, Kanali Gaddafi na familia yake kusalia nchini humo, Ghoga amesema hilo haliwezekani.

Msemaji huyo wa upinzani amesema, kwa sasa hakuna mzozo wa kijeshi nchini humo.


Amesema kuongezwa kwa mashambulio ya anga yanayofanywa na wanajeshi wa NATO, kumeimarisha hali kwa waasi wanaopinga serikali ya Gadaffi.

Huku hayo yakijri, mtengenezaji filamu mmoja aliyeteuliwa kuwania tuzo la filamu maarufu kama Oscars, ameuawa mjini Misrata.



Tim Hetherington
Tim Hetherington, ambaye ana uraia wa Uingereza na Marekani aliuawa kwenye shambulio kati kati mwa mji huo ambao umeendelea kushuhudia mapigano makali kati ya wanajeshi watiifu kwa Kanali Gaddafi na wale wa waasi.

Hetherington alikuwa mmoja wa wasimamzi wa filamu ya Resrepo iliyotengenezwa kuhusu vita vya Afghanistan.

Filamu hiyo iliteuliwa kuwania tuzo la oscar mwaka huu.

Mwandishi mwingine Chris Hondros, raia wa Marekani ambaye alikuwa miongoni mwa waliojeruhiwa kwenye shambulio hilo, aliaga dunia akipokea matibabu hospitalini.

Ripoti zinasema mwandishi mwingine wa habari pia alijeruhiwa kwenye shambulizi hilo

No comments:

Post a Comment