KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, February 19, 2011

Sehemu ya mitambo ya Songas yaungua


MTAMBO mmoja wa kuzalisha umeme ya kampuni ya Songas uliyoko Ubungo jijini Dar es Salaam umeungua kwa moto.
Moto huo ulianza katika mtambo namba tatu kwenye majira ya saa 8 mchana jana

Hata hivyo moto huo uliwahiwa kuzimwa na kampuni ya zimamoto ya Knight Support na haukuwahi kuleta madhara makubwa.

Katika tukio hilo la kuungua moto hawakuonyesha ushirikiano na vyombo vya habari na waliofika hapo walizuiliwa kuingia ndani na baadhi ya wenye madaraka eneo hilo hawakuonyesha ushirikiano kuzungumzia suala hilo

No comments:

Post a Comment