KARIBU MAISHANI
KARIBU MAISHANI
Saturday, January 29, 2011
Uganda yatoa hadhari ya kufanyika ugaidi
Polisi nchini Uganda wametoa hadhari mpya dhidi ya kutokea tukio la kigaidi. Hadhari hii imetolewa wakati huu wakati uchaguzi mkuu ukiwa unakaribia.
Polisi wa Uganda
Mkuu wa polisi nchini Uganda Meja Jemedari Kale Kaihura ametoa onyo la kutokea shambulio la kigaidi na hivyo kuwapa hadhari wananchi.
Maelezo zaidi ni kuwa tisho la shambulio la kigaidi linatokana na kundi la Al Shabaab na linapangwa siku za mwisho za kampeni pamoja na uchaguzi.
Kampeini za Urais na Ubunge zinaendelea na zimepangwa kumalizika tarehe 16 mwezi huu wa Februari na uchaguzi utafanyika tarehe 18 mwezi huu wa Februari.
Polisi wametoa hadhari kwa wananchi kuwa waangalifu na kuripoti watu wasioeleweka kwa vyombo vya usalama, pamoja na vifurushi ambavyo wanashuku vikiwa vimeachwa mahali
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment