KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, January 29, 2011

Misri waanza mazungumzo

Baada ya wiki mbili za maandamano ya kuipinga serikali nchini Misri, makamu wa Rais Omar Suleiman ameanza mazungumzo na makundi ya upinzani
Waandamanaji wakimiminika kwenye uwanja wa Tahrir, Cairo


Miongoni mwa wanaoshiriki kwenye mazungumzo hayo ni lile la Muslim Brotherhood na waakilishi wa vijana, ambao ndio wamekuwa wakiongoza maandamano.

Taarifa zinasema tayari makubaliano yamefanyika ya kuunda kamati ya kuchunguza mabadiliko yanayotakiwa kufanyika katika katiba ya nchi hiyo.

Kundi la Muslim Brotherhood ambalo bado limepigwa marufuku nchini Misri lilikuwa limesema linasubiri kuona ikiwa serikali iko tayari kufanya mabadiliko ya kisiasa mara moja.

Kundi la Muslim Brotherhood

Bado linamtaka Rais Mubarak ajiuzulu, na linasema ni sharti serikali ya muungano iundwe, na pia sheria za dharura zibadilishwe.

Hii ni mara ya kwanza kwa serikali ya Misri kufanya mazungumzo na kundi hilo la Muslim Brotherhood lililopigwa marufuku.

Makundi ya upinzani yanataka Bw Mubarak kujiuzulu mara moja lakini amesema kuondoka kwake kwa dharura kutaleta vurugu.

Aidha, amesema hatagombea kiti cha urais katika uchaguzi utakaofanyika mwezi Septemba.

Wakati huo huo, benki zilizokuwa zimefungwa kwa zaidi ya juma moja zimefunguliwa huku kukiwa na wasi wasi kwamba watu wengi watatoa pesa zao kutoka benki kufikia kiwango kikubwa mno.



Raia wantoa pesa kutoka benki

Uchumi wa Misri umeumia kutokana na maandamano dhidi ya Rais Mubarak, na serikali ina hamu ya kuona nchi ikirudi katika hali ya kawaida.

Halaiki ya watu wamekuwa wakiandamana katika mitaa ya Cairo na miji mingine majuma mawili yaliyopita wakitaka mabadiliko katika mfumo wa demokrasia.

Kabla ya mazungumzo msemaji wa Muslim Brotherhood, Mahmoud Azzat, alisema wakuu wameanza kukubali shuruti zao.

Lakini maandamano yanaendelea leo katika medani Tahrir mjini Cairo.

No comments:

Post a Comment