KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, January 29, 2011

Mauaji ya Kato yazusha hisia mchanganyiko



David KatoMauaji ya mwanaharakati wa kutetea haki za mashoga, David Kato, yaliyotokea jana nchini Uganda, yamezua hisia tofauti duniani kote, ikiwa ni pamoja na mashirika ya kutetea haki za binadamu, yakihusishwa na msimamo wake.

Hata hivyo, taarifa za mwanzo za uchunguzi wa polisi, zinaonesha kuwa huenda mwanaharakati huyo alivamiwa na wezi akiwa nyumbani mwake.

Mkuu wa polisi wa Uganda, Kale Kayihura, anasema mauaji hayo hayajahusiana na harakati za marehemu Kato, aliyekuwa na msimamo mkali dhidi ya sheria za kuwabana watu wanaofanya mapenzi ya jinsia moja, kama taarifa ya Leyla Ndinda inavyosimulia kutoka Uganda

No comments:

Post a Comment