KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, December 30, 2010

Siku ya wapendanao

Siku ya wapendanao ni sikukuu ambayo huadhimishwa kila ifikapo tarehe 14 Februari ya kila mwaka (Valentine Day).

Historia yake imeanzia karne ya 3 huko Roma ambapo alikuwapo mtakatifu valentine au Valentinus. Kaisari wakati huo alikuwa Claudius II yeye aliona kuwa askari mkakamavu na bora zaidi ni yule asiyeoa wala kuwa na familia (kapera).
Hivyo alipiga marufuku ndoa kwa askari. Mtakatifu Valentinus alipinga jambo hili hivyo kuendelea kufungisha ndoa kwa siri. Mfalme Claudius alipopata habari hizi aliamuru kukamatwa kwa Valentinus na kuuwawa.



Kuna hadithi ya kuwa akiwa gerezani mtakatifu Valentinus aliandika barua ambayo ilikuwa na salamu za kwanza za valentine kwa binti aliyekuja kumsalimia gerezani, mwisho wa barua alihitimisha kwa maneno haya (From your Valentine). Toka hapa valentine anakumbukwa kama mtetezi wawapendanao na siku hii kuadhimishwa kote duniani

No comments:

Post a Comment