KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, December 30, 2010

Mti wenye thamani zaidi




Hoteli moja mjini Abu Dhabi, katika Falme za Kiarabu imetengeneza mti wa Krismasi, wenye thamani zaidi duniani. Mti huo una thamani ya dola milioni kumi na moja.

Mti huo umepambwa na vito vya thamani ikiwa ni madini na taa za kuvutia za rangi mbalimbali. Taarifa zinasema mti wenyewe tu unathamani ya dola milioni kumi, na madini na vito vya thamani ndio vimeongeza thamani hiyo na kufikia milioni kumi na moja.

Meneja mkuu wa hoteli hiyo Hans Olbertz amesema kila mwaka huwa wanaandaa mti wa Krismasi, lakini mwaka huu wanataka kufanya kitu tofauti. Meneja huyo amesema wanawasiliana na taasisi ya Guiness ya rekodi za dunia, kuona kama mti huo utavinja rekodi ya kuwa mti wa Krismasi wenye thamani zaidi dunaini.

Mapambo katika mti huo ni pamoja na Mikufu na saa za thamani, almasi, na lulu, pamoja na mawe mengine ya thamani. Mti huo umewekwa katika baraza kubwa la hoteli ya Emirates Palace yenye vyumba mia tatu na mbili.

Alipoulizwa kuhusu ulinzi wa mti huo, Hazem Harfoush amesema mti huo ni uthibitisho kuwa Abu Dhabi ni salama. Na hoteli hiyo ni salama zaidi Bwana Harfoushameiambia BBC. "tuna walinzi hapa saa ishirini na nne, walinzi wanne, pamoja na camera za ulinzi.


--------------------------------------------------------------------------------

No comments:

Post a Comment