KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Thursday, November 11, 2010

Mwana Mfalme William kuoa





William, ambaye ni mrithi wa pili wa kiti cha ufalme, atafunga ndoa mwakani, katika mwaka ambao ungeadhimisha miaka 30 ya ndoa ya wazazi wake.

Wawili hao waliweka ahadi ya uchumba mwezi Oktoba nchini Kenya, wakati wakiwa katika mapumziko.


William na Kate walianza kuwa na mahusiano miaka minane iliyopita, wakati wakisoma katika chuo kikuu cha cha Mtakatifu Andrews huko Fife, ambapo pia waliishi katika nyumba moja.

Ndoa hiyo imetangazwa katika taarifa fupi iliyotolewa na Clarence House.

Taarifa

Taarifa hiyo imesema: "Mwana Mfalme wa Wales, ana furaha ya kutangaza ndoa ya mwanae, Mwana Mfalme William atakayofunga na Bi Catherine Middleton.

"Harusi itafanyika wakati wa majira ya joto ya mwaka 2011, mjini London. Taarifa zaidi kuhusu harusi hiyo zitatangazwa baadaye.

"Mwana Mfalme William amemfahamisha Malkia na ndugu wengine wa karibu.




"Mwana Mfalme William pia ameomba ruhusa kutoka kwa baba wa Bi Kate.

"Baada ya kufunga ndoa, wawili hao wataishi kaskazini mwa Wales, ambapo Mwana Mfalme William ataendelea na kazi katika jeshi la Anga la Uingereza Royal Air Force."

No comments:

Post a Comment