KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, November 27, 2010

Magufuli aanza kazi kwa moto, aagiza wakandarasi wasiofaa wafukuzwe nc


NI SIKU moja toka Rais Kikwete kuwaapisha Mawaziri, Waziri wa Ujenzi,Dk. John Magufuli ameanza kazi rasmi jana na kuzungumza na watendaji wakuu wa wizara hiyo na kuwakabidhi ilani ya Chama cha Mapinduzi huku akitoa maagizo yake yatekelezwe mara moja
Waziri Magufuli aliwataka watendaji wakuu na wakuu wa idara katika wizara hiyo, kufanya kazi kwa bidii na atakayeonekana mzembe atafukuzwa kazi mara moja bila hata ya kuoneana aibu wala huruma.

Hayo aliyasema jana jijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza na watendaji hao kuwataka wawe makini na wajiandae kufanya kazi kwani katika miaka mitatu ya mwanzo ni utekelezaji na miwili ya mwisho ni kukamilisha kazi zzote za wizara hiyo.

KAtika kiako hicho Magufuli alitaka wakandrasi wote wabobu kufukuzwa nchini hasa wale wanaochelewesha ujenzi wa barabara kama ya Mandela, uwanja wa ndegew a Songwe na kuwa kero kwa wananchi.

“Lazima wakandarasi hao waondoke na wafutiwe mkataba na hata wakikibmilia nchi jirani tutawasiliana na mawaziri wakuu wan chi hizo” alisiema Magufuli.


Pia Magufuli alishangaa ni kwanini ujenzi wa daraja la Kigamboni unacheleweshwa, hivyo aliagiza lijengwe haraka na kama Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) wameshindwa kazi hiyo watoe ripoti haraka ili liweze kufanyiwa kazi.

Waziri MAgufuli ameahdidi kumaliza tatizo la msongamano wa magari barabarani kwani wizara hiyo itahakikisha watajenga barabara za angani (Flyovers).


Pia aliagiza kitengo cha ujenzi kuweka kivuko cha kuanzia Kivukoni hadi Tegeta ili kupunguza msongamano wa wananchi wanaokesha barabarani.


Pia alitoa mwezi mmoja kwa wale waliokopeshwa nyumba za serikali na hawajamaliza kulipa madeni hnayo, aliwataka waandikiwe barua za kutakiwa kumaliza madeni hayo na katika muda utakaowekwa wasiomaliza madeni wafukuzwe katika nyumba hizo kwani wataona wanabembelezwa na hawaoni wanafanya makosa kukalia nyumba hizo za serikali bila kuzilipia.

Pia Waziri Magufuli alishukuru kwa kupewa msaidizi wake, msoni Mwakyembe kwa kuwa ni mchapa kazi hodari wataweza kuiongoza vyeema wizara hiyo.

“Halafu nyinyi watendaji mmekalia majungu tu hapa wizarani, sasa miaka hii mitano ni yakufanya kazi, hakuna kuoneana aibu wala kuogopwa kurogwa” alimalizia Magufuli

No comments:

Post a Comment