KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Friday, November 19, 2010

HOSPITALI ya Mwananyamala inakabiliwa na ukosefu wa huduma ya maji


HOSPITALI ya Mwananyamala inakabiliwa na ukosefu wa huduma ya maji, na kufanya mazingira kwua magumu ndani ya hospitali hiyo kutokana na tatizo hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Kaimu Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Dk. Kariamel Wandi, alisema kuwa kwa sasa hospitali hiyo kubwa I nakabiliwa na tatizo la maji inayopelekea huduma kuwa dhaifu katika baadhi ya wodi kwa kuwa maji ni muhimu ndani ya wodi hizo.

Alisema hali inaonekana kuwa tata zaidi hasa katika wodi ya wazazi, upasuaji kwa kuwa maji huwa yanatmika wka wingi kutokana na aina yaw agonjwa hao.

Alisema hasa tabu inakuwa ngumu kaitka wodi ya wazazi wka kwua kwa siku wanapokea idadi kubwa ya akina mama wanaokuja kujifungua na idadi inaweza kufikia kupokea akina mama 100 ka siku moja.

Hivyo kutokana na tatizo hilo uongozi wa hospitali hiyo ya wilaya ya Kinondoni wapo kwenye juhudi za kusambaratisha tatizo hilo na ikishindikana wataweza kuifunga hadi hali ya maji itengemae

No comments:

Post a Comment