KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, November 27, 2010

Hasara ya mabilioni yakadiriwa Sudan



Uchumi wa Sudan huenda ukaathirika vibaya ikiwa vita vitazuka upya kati ya kusini na kaskazini
Utafiti kuhusu athari za kiuchumi zitakazotokea ikiwa vita vya wenyewe kwa wenyewe vitaibuka nchini Sudan unaonyesha kuwa taifa hilo na jirani zake litapata hasara ya $100 bilioni.

Ripoti iliochapishwa na baraza la ushauri wa maswala ya kiuchumi la Frontier Economics, inafichua kuwa iwapo kura ya maamuzi kuhusu uhuru wa Sudan Kusini itasababisha vita, huenda hasara ya asilimia thelathini na nne ya pato la kitaifa la Sudan katika kipindi cha miaka kumi ikashuhudiwa.

Wadidisi kutoka baraza hilo la kiuchumu, wameongeza kuwa uchumi wa nchi jirani kama vile Kenya na Ethiopia huenda ukapoteza dola bilioni moja kila mwaka baada ya vita kuanza.

Wakaazi wa kusini mwa Sudan, eneo lenye utajiri mkubwa wa mafuta wanatarajiwa kupiga kura ya kuunga mkono mpango wa kujitenga na kaskazini mwezi Januari mwakani.

Wachambuzi wanasema mzozo mpya utazuia wawekezaji kuingia nchini Sudan, utaongeza garama ya kijeshi na kuleta uhaba wa fedha za misaada wa kibinadamu

No comments:

Post a Comment