KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Monday, November 1, 2010

CUF yaongoza matokeo ya awali Buguruni



MATOKEO ya awali ya Uraisi , Ubunge na Madiwani Chama Cha Wananchi [CUF] kinaongoza kwa ushindi wka matokeo ya awali katika vituo vya Buguruni A na B.
Katika kituo cha Buguruni A matokeo ya urais yameonyesha CUF kupata kura 420, CCM kura 402 CHADEMA kura 239, NCCR 0 na TLP 0

Kwa upande wa ubunge CUF imepata kura 356, CCM kura 341 CHADEMA 160, NCCR 0 na TLP 0

Hivyo kwa matokeo hayo yaliyopatikana jana majira ya saa 4 usiku, katika kituo hicho chama cha CUF kimeonekanea kuongoza kwa kura katika maeneo ya Buguruni A na B.

Nifahamishe pia ilishuhudia wakazi wa maeneo hayo wake kwa waume,wakiwa wameweka vikundi kwa madai ya kuwa wanalinda kura zao huku wengine wakionekeana kuwa na hasira kali huku wengine wakibishana na askari wa jiji kuamriwa kuondoka maeneo hayo

No comments:

Post a Comment