KARIBU MAISHANI

KARIBU MAISHANI

Saturday, November 27, 2010

China yatoa pendekezo mzozo wa Korea


Huku mvutano ukiendelea baina ya Korea Kaskazini na Kusini, China imetoa wito kufanyike mazungumzo ya dharura, baina ya mataifa sita yaliyohusika na upatanishi katika mpango wa nuklia wa Korea Kaskazini.


China yavalia njuga kumaliza mzozo wa Korea


Afisa mmoja wa China, aliwaambia waandishi wa habari mjini Beijing, kwamba China ina wasiwasi mkubwa kuhusu yaliyotokea hivi karibuni katika Rasi ya Korea na inataka mataifa sita, Marekani, Urusi, Japani, China yenyewe na Korea mbili, yakutane mwanzo wa mwezi ujao.

Lakini Korea Kusini imesema huu si wakati wa kurejea tena kwenye mazungumzo ya pande hizo sita

No comments:

Post a Comment